Jeshi la Polisi leo limethibitisha kuwa linawashikilia watu wawili kuhusiana na kujihusisha na mtandao wenye kukashfu watu na unaowezekana kabisa kuwa ni wa kihalifu. Hayo yamesemwa na Inspekta Jenerali wa Polisi Bw. Said Mwema leo akizungumza na waandishi wa habari Jijini Dar-es-Saalam. Msemaji wa polisi amedai kuwa mtandao huo unahusiana na ughaidi.
Bila kutaja majina ya wale inaowashikilia, Bw. Mwema alisema kuwa maendeleo ya sayansi na teknolojia yanawezesha watu kuanzisha mitandao mbalimbali ambayo mingine inawezekana kuwa ni ya kihalifu. Bw. Mwema amesema kuwa matumizi mabaya ya teknolojia hiyo ya mawasiliano ya kiintaneti imesababisha baadhi ya watu kutumia mtandao huo kufanya mambo ya kihalifu. Alidai kuwa baadhi ya taarifa zinazoandikwa Jambo Forums zinagusa watu binafsi na akadai kuwa mitando ya namna hiyo "isitumike kama vivuli vya kutenda uhalifu". Alipoulizwa na mmoja wa waandishi wa habari kutaja ni mada gani iliyowachafua watu binafsi ambayo imesababisha vijana hao wakamatwe alishindwa kufanya hivyo na kudai kuwa "uchunguzi" bado unaendelea na ya kuwa bado wanashikirikiana na wale waliolalamika kuwa wanachafuliwa ili wawaeleze ni kitu gani hasa kinaendelea. Hata alipoulizwa kutaja majina ya wanaowashikilia alikataa kufanya hivyo. Muda mfupi baadaye jitihada za kumpata Mkurugenzi wa Makosa ya Jinai Bw. Robert Manumba zilishindikana hasa baada ya kudaiwa kuwa alikuwa ameitwa "Ikulu". Haijulikani kama wito huo unahusiana kwa namna yoyote na tukio la kukamatwa kwa vijana hawa ambao mmoja wao bado ni chini ya miaka 21. Wakati huo huo, Mwanachama Mwandamizi wa Jambo Forums Bw. M. M. Mwanakijiji anatarajiwa kuzungumza na shirika la Utangazaji la BBC Idhaa ya Kiswahili baadaye leo mchana kwenye kipindi cha "Dira ya Dunia" kujadili sakata hilo la vyombo vya serikali kujaribu kusambaratisha mtandao wa JF huku mtandao wa waliokula fedha za Benki Kuu, walionunua Rada,na waliotuletea majenereta ya mazingaombwe ukiendelea kudunda. Mmoja wa mashabiki wa JF kutoka Kiwalani jijini Dar na mfanyakazi wa taasisi moja nyeti nchi na ambaye ni mwanachama wa Jambo Forums ameiambia KLH News kuwa inasikitisha kuwa wahalifu waliochota fedha za umma wanaendelea kudunda mitaani, "mimi nilitarajia watu kama kina Gray Mgonja ndio wangekuwa kwenye selo za Polisi au wale kina Jeetu Patel na Vithlani, lakini nashangaa wanaenda kukamata vidagaa ambavyo hata kuvitafuna havijai kinywani". Naye Mhadhiri Mwandamizi wa Sheria katika Chuo Kikuu cha Dar-es-Salaam ambaye aliomba asitajwe jina lake ameiambia KLH News kuwa "Polisi hawana kesi, wanajaribu kutishia tu watu wenye mawazo tofauti na serikali. Ni jaribio la kuzima uhuru wa maoni kwa vile JF iliibua kwa uwazi zaidi mambo ya Richmond na Buzwagi". Vijana waliokamatwa bado wako nje baada ya kupewa dhamana na Mwanasheria wao Bw. Tundu Lissu anaendelea kufuatilia ili kuona kuwa haki zao za Kikatiba hazikuvunjwa wakiwa mikononi mwa Polisi. Jumuiya mbalimbali za wananchi na vyama vya kisiasa vinatarajiwa kutoa matamko mbalimbali kuhusiana na suala hili. Wakati huo huo KLH News bado inatoa wito wa wananchi kusaidia timu ya wanasheria na "Invisible" ambaye anahangaika kuhakikisha kuwa JF inarudi kwa namna moja au nyingine. Kwa anaetaka kusaidia anaweza kutumia link ya Paypal iliyoko kwenye http://www.mwanakijiji.podomatic.com au kupiga simu 1 248 556 6748 ofisi za KLH news. Views: 5748 | Print | E-mail
1. Hii ndiyo njia Written by mtembezi, on 20-02-2008 16:52 Naam baada ya Mwema IGP kutamka bayana (maneno aliyowekewa kinywani) kuwa JF ni mtandao wa kihalifu basi hii ndiyo njia ya promotion kwa jamii ambapo serikali imeifanya bila gharama yoyote kutoka kwetu. Naamini kuwa sasa rasmi JF itakuwa ktk vinywa vya watanzania na ita hit ktk headings mbalimbali bila uoga wowote. Nawatia shime culumnist wa JF wekeni post zenu ktk vyombo vya habari kulaani ubabe wa kipolisi dhidi ya mtandano wa JF. wajue kuwa bila JF white head asingechumpa kutoka alipokuwa. AKA Msanii |
2. watawala wasio na maono Written by kuti kavu, on 20-02-2008 16:55 Hivi kweli jeshi letu linakubali kutumiwa na mafisadi kiasi hiki cha kuudhihirishia umma wa watanzania na ulimwengu kwa ujumla,bila aibu na kuwaacha watuhumiwa wa wizi wa mali ya umma wakitanua mitaani bila aibu. Kwa kweli hili linasikitisha sana,tunajua mwena analinda maslahi ya mabwana zake na kuwacha watanzani wakiteseka bila huruma,basi sasa ndio kazi imeanza nilazima tuhakikishe watanzania wanaondokana na ukandamizwaji wa mafisadi na dhuluma ya aina yoyote ile. |
3. Mnyonge Mnyongeni, Haki yake mpeni Written by Morani75, on 20-02-2008 16:57 Kaazi kweli kweli pale wanapoamua kuweka sheria zisizokuwepo, eti sheria ya 1971 wakati wa karne ya mtandao!! Duh, Mungu Ibariki Tanzania na watu wake........... |
4. Written by Mtu Kwao, on 20-02-2008 17:08 UWWIIIIII UWIIIIIII Jamani mwema nae katekwa na mafisadi na kuwa kwake kote kwenye inerpol .kweli njaa zitaponza watu wengi sana.yani kweli mwema kadiriki kutunga uongo kuhusu jambo forum ?sasa wameamua kuigeuza mtandao wa kihaliu kweli siasa mchezo mchafu.sasa na hao waliosema wamechafuliwa majina ni akina nani mbona mwema anaogopa kuwataja?Jamani mapambano ndio yameanza na kamwe hayataisha bila ya haki ya watanzania walio wengi kupatikana kuliko huo mtandao wa kifisadi ambao watu wake wnahesabika. |
5. Wanachekesha Hawa Written by Baba Winne, on 20-02-2008 17:17 Kaka Mwema na rafiki yangu wa karibu Mtweve sikutarajia hata siku moja mtachukua maamuzi ya kiimla namana hii. Inasikitisha sana kwa kuona wasomi kama ninyi mnaweza kuchukua uamuzi wa kiimla naman hii. Mtweve nakumbuka enzi zetu pale mlimani wakati wa shukle yetuu ya uzeeni ulikuwana busara sana hebu tumia busara hiyo kuepukana na hawa mafisadi wanao taka kukutumia wewe na bosi wako ndugu yangu. Nitakutafuta personally tutete ni aibu kubwa. Wakamateni hao akina Fisadi Lowasa, Bilali ................... |
6. ukuzwaji Written by DAR si LAMU, on 20-02-2008 17:18 ..ukuzaji mambo [mtandao wa kihalifu?],huwafanya watu kuwashangaa watu kama hawafahamu au hawajui. kimya huwa ni busara pale pasipo na uhakika. ..generational gap ni tatizo kubwa. |
7. Written by Mtu Kwao, on 20-02-2008 17:26 Wanachekesha kidogo kwani Mi sipati picha labda nyie wakubwa akina baba winne mkisema mtasikilizwa mana wanaona huu mtandao ni wa kihalifu na si wa ukweli tupu.hizi kwenye hiki kiapo sha polisi hakuna mahali wanasema nitatenda kweli daima?kama papo basi wabadilishe mana polisi siku ni wabambikiaji watu kesi kama hizi.USHINDI NI LAZIMA KWA GHARAMA YOYOTE WAPENDA HAKI WA JAMBO FORUM |
8. NIMEICHOKA CCM, HAITADUMU Written by Msanii, on 20-02-2008 17:30 Ndugu Zangu wa JF na KLHN Nimesikitishwa sana na uhalifu unaofanywa na polisi dhidi ya watanzania, nakupongeza kwa kuchukua hatua ya kufuatilia, ninaamini kama kukamatwa tupo wengi tutakao wekwa ndani, Ninatangaza rasmi kuomba kurudisha kadi yangu ya CCM ambayo niliikata mwaka juzi (nilikuwa kipofu) Ni aibu kwa chama changu kilichopo madarakani kufanya mambo ya kipuuzi kama haya na ninakataa uhuni huu kwa nguvu zote. |
9. Written by Neema, on 20-02-2008 17:34 jamani sikilizeni bbc wameshaitoa kwenye heading za dira ya dunia |
10. Written by JAMBOFORUMS WINS WINS WINS, on 20-02-2008 17:35 Walianza eti ni udaka wa kwenye mtandao, sasa chombo cha uhalifu, wats next chama cha siasa, then terrorits...ni aibu watu wazima serikalini kutamka maneno yasiyokuwa na mwelekeo..aibu Mwema kumbe wewe kama Mahita...TUMEKWISHA!!! Hizo baacha za mafisadi utakula utaoza utaanza mamilioni ya watanzania maskini na kufa njaa...tumia uongozi wako kwa akili with the peoples interests at heart sio mafisadi..aibu sana... sasa tutaweka yako wazi..tuone ... |
11. Network error Written by Msanii, on 20-02-2008 17:41 Nitakuwa off kwa muda kwani ninaenda kufomart pc na laptop baada ya kushambuliwa na spyware wanaozitafuna bila nafasi. Nipo alert na kama kuna chochote kitanitokea JF member aitwaye Mtu atawasiliana na Mnyika na wengineo. Sina hofu ninatembea kifua mbele na JF yangu moyoni, walah hiki ndicho kipindi tungevaa tsht zetu wakome mafisadi. Nitakuwa nafuatilia maendeleo yetu na ninaombea JF irudi hewani, ninakubaliana na wazo la mmoja wetu awali aliyesema tusiingie ktk blog zingine zaid ya website hii maana naamin zitaanzishwa jamboforums kibao ili kujaribu kutuweka karibu na manyang'au wa kifisadi. tutulie hapa kujua kitakachojiri na hatua zipi za kizalendo tutazifuata kuhakikisha Tanzania inapata mwelekeo sahihi. |
12. haya ni mambo ya Pinda Written by mwenye uchungu, on 20-02-2008 17:53 nakumbuka mwafrika wa kike alisema kuwa Pinda ni mwanausalama na amekuja kwa kazi maalumu ya kukomesha uvujaji wa siri za serikali na wengi hapa tukamcheka vile anavyochemka mara kwa mara. nimeanza kuogopa baada ya haya yanayotokea na imepita masaa 24 sijamuona hapa KLH. Mwanakijiji jamani fuatilia ujue kama MWK yuko salama au naye tayari wamemkubenea. Serikali ya Pinda imeanza kutisha jamani hivi tutafika kweli? |
13. Fikra Mgando Written by Ushirombo, on 20-02-2008 17:55 WanaJF wenzangu!! Hii ni aibu kubwa kwa IGP Said Mwema kuongelea kuwa JF ni tovuti ya kihalifu kwa kuwa inakashfu watu, ninani aliyeenda mahakamani kulalamika kuwa amekashifiwa ama kudhalilishwa? Lowassa..Rostam, Karamagi ama mama Meghji? Ningeelewa kama jeshi lake ningewakamata akina Gray Mgonja, Balali, Mkapa kwa kuiba pesa za watanzania na kusababisha ugumu wa maisha ....Kama utapitia hapa tunakuomba uachane na fikra mgando badilika karne hii ni tofauti na zama za mawe...hapa unasaidia kuitangaza JF kirahisi Ushi wa Rombo |
14. BBC Written by Msanii, on 20-02-2008 17:56 Mwanakijiji ndiyo yuko hewani dira ya dunia mda huu?? Jamani nawatakia mapambano mema, mie ninasign off till next time |
15. watakamata wangapi? Written by rwabugiri, on 20-02-2008 17:57 Nahisi hapa hawa mafisadi wana ipromote JF kinyume nyume wakidhani wanaimaliza! Naamini ikijaliwa rudi hewani itakuwa maarufu saba mara sabini kuliko ilivo kuwa sasa. Tazama sasa JF ina paa BBC!! Long live JF, washindwe wote wenye nia mbaya juu yako!. Hii ni sauti ya walio wengi, sauti ya mafisadi haiwezi shinda sauti ya MUNGU! |
16. MICHANGO INAWASILISHWAJE???? Written by NYAMBALA, on 20-02-2008 18:03 Mwanakijiji pls tujulishe namna ya kuwasilisha michango especially kwa sisi tuliopo hapa nyumbani! |
17. Michango inapitia hapa Written by KAS, on 20-02-2008 18:13 Kwa wanaotaka kutoa michango. Kuna link ya paypall kwenye www.mwanakijiji.podomatic.com na utaweza kutoa mchango wako. |
18. Written by KAS, on 20-02-2008 18:18 Ujinga mtupu anaosema msemaji wa polisi. Hii nchi inapelekwa siko ndiko. Ushindi lazima upatinakane. Mnakumbuka enzi za issues ya Zitto nayo ilikuwa hivi hivi. Issue hii itawagaeuka kama ile ya Zitto badala ya kuuangamiza mtandao wa JF watakuwa wame ufanyie matangazo sasa hata mtu aliyeko Ileje anayesikiliza BBC anajua JF ni nini. Mafisadi wakubwa hawa. Mie natamani kumvamia mtu kwa magumiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiii |
19. kituko Written by Msanii, on 20-02-2008 18:32 nimebidi kurudi hewani baada ya kumsikia Mgass MC wa polisi kuhusu sakata la vijana wa JF. Amejiumauja saaana ktk kuongea na hakuna point hata moja maana tangu aulizwe kwanini wamewakamata vijana wa Jf anaanza kutoa historia ya mitandao ambayo hata hajui ni nin. Wamesema kuwa wnaifuatilia motandao mingine, just angalizo kwa Mzee mwanakijiji kuwa awe alert na aongeze ulinzi hakika ktk ID zetu humu. Nadhani nina angalizo la kuchungulia hapa, Just iwenawezekana baada ya TIS kuitumia JF kumwaga radhi hadharani kuhusu mambo yaliyojificha ya sirikali sasa taasisi hiyo inaona lengo limetimia na inataka kuifunga forum hii. Hivyo kama invisible ananipata huko aliko ni vyema akawa makini zaidi kwani hawa jamaa wanataka kulikuza tukio hili lionekane la kihalifu zaidi. Hata mkoloni aliwtumia watanzania wenzetu kutukandamiza. JAMANI NI ANGALIZO TU. |
20. Written by mkuu, on 20-02-2008 18:38 Tunashukuru sana mkuu wa polisi kwa hii free promotion na tafadhari tusitishiane maisha.....sasa nafikiri wanataka tuwafanye walichomfanya waziri wa Liberia,hii vita wanajisumbua tuu wataishia kuaibika tuu,sasa naona ndio kumekucha,wakuu unajua mpaka sasa hivi hatujui kwanini JF haipatikani,tunaomba maelezo ya kueleweka tafadhari |
21. Written by mtuwapwani, on 20-02-2008 18:40 Hawa kweli mbumbu mtandao wa kigaidi huyo bush mwenyewe hajawahi kuukamata na kama mitandao ya kigaidi inakamatika basi..wasingepata tabu na magaidi...sasa wee waache sasa utafunguliwa..huo utakua kama wa kigaidi utawaanika kweli kweli na ufisadi wao |
22. JF forever Written by mzee wa chini, on 20-02-2008 18:53 ni wakati tu wa mpito...this is the time for JF to sppeed up...ni nauhakika hawa viongozi waliongo'lewa madarakani wote hawakufurahia......also inawezekana huyu PM wetu mpya alijua kilakitu kinavyoendelea ila alisubiria tu apate madaraka ila afanyizie....hatutakubali kufanya ndondocha....wamekula vya kutosha...... Mungu yupo kupigana na wale wapenda haki siku zote..so no matter how polisi will do at the end itakuwa ni kuaibika wenyewe..... |
23. JF Siku zote itakuwepo by any" MEANS" Written by BabaH, on 20-02-2008 19:37 Kweli nimeamini Tanzania viongozi wengi ni watupu tena sana tu Yaani ni kwa kigezo kipi huyo Mwema anasema JF ni ya kigaidi?? hilo Jeshi kweli linakitengo cha uchunguzi, kilichokamilika, Kama kipo nina wasiwasi sana na Jeshi letu na Polisi, kwa tutoa habari za Ugaidi na kusihusisha na JF Poleni wanachama wenzangu lakini nina imani tutashinda kwa njia yoyote ile. |
24. Sasa ndo kazi imeanza.. Written by Simbajike, on 20-02-2008 19:43 Sasa yale maandiko yanatimia kuwa kuna siku CCM na wafuasi wake wataishiwa sera. Yaani sera-sifuri. Wameanza kukamata na kutuhumu teknolojia. Mwema nae ameanza kubeba aibu za Mwanyika na Hosea sasa. Mkubwa mzima anapambana na asiowaona... ila poa tu tutafika Sasa hii promo ndio itawamaliza maana hata wasiojua JF watapenda kuijua. Kudadek..Strategist wao ameboil kinomi.. |
25. Written by Mtu Kwao, on 20-02-2008 19:53
mI Nilidhani msemaji wa polisi ataongea kitu cha maana kumbe naye ni maneno ya kukariri tu toka enzi zile .hivi hawa wanajua mtanado wa kigaidi kweli?mana wanafurahi tu kusema ugaidi wakati hakuna kitu kama hicho jambo forum.oo mara mtandao unasambaza picha za ngono mara nini .Mi nashauri huyu baba na mtoto wake wamalizane wenyewe watuachie jambo forum yetu.Nisaidieni nimesikia manumba akisema dar walikamata watu wwili wakijihusisha na ugaidi wakati wa ujio wa bush.sasa wanataka kusema ni hawa wana jf au? |
26. JF poleni na hongeni.. hii changamoto! Written by Mzalendoi, on 20-02-2008 19:59 JF will never be the same again- all this will pass- and JF will be more famous! Tupo pamoja! Viva JF Viva!!! |
27. Written by John Mnyika, on 20-02-2008 20:03 Teh teh teh: Tamko nililolitoa leo kwa kale kanafasi kangu kengine linapatikana hapa: http://www.chadema.net/blogu/mnyika/2008/02/kwa-niaba-ya-baraza-la-vijana-wa.html Tuendelee kuwashika! Mpaka Kieleweke. Nimekosa mahojiano ya mwanakijiji, najiuliza- ni kwanini polisi wamekwepa kutaja majina ya waliyowakamata pamoja na kuwa toka jana yalishakuwa hadharani kwenye mtandao? Kaka "invinsible" hebu turudishieni JF hewani tafadhali, achaneni na vitisho vya mafisadi. WanaCCM mlio wanachama wa JF ikiwemo serikalini, hebu washaurini wenzenu wasiliabishe taifa kwa maamuzi ya kiimla! JJ JJ |
28. Naomba namba ya simu ya Mwema please Written by BabaH, on 20-02-2008 20:10 Jamani kuna mtu anayo namba ya simu ya Said Mwema, ninaomba kama kuna mtu anayo, uzalendo umenishinda nataka kuongea nae Kama nakamatwa poa tu bwana, Mandela alikamatwa na wazungu na akasota Jela miaka kibao ndo hawa akina Mwema!!! Please naomba nipewe namba maana nataka kuongea nae laivu nimuulize kweli ana uchungu na hii nchi na ni vigezo gani wanavyotumia kayika uchunguzi wao. Maana uchunguzi hauwapati Mafisadi, ila unawakama watu wanaoipenda nchi yao Nisaidieni please Tuko pamoja jamani |
29. KWA KWELI SASA POLISI WAMEKOSA KAZI Written by Mbongo murua, on 20-02-2008 21:24 Wakuu wana jf kwa kweli jeshi la polisi limekosa kazi,kuhusisha jf na ugaidi.Hivi polisi ugaidi wanaujua?ina maana sisi watu wote tunaochangia mule jf tuna msimamo wa aina moja?mbona tunatoa hoja na kupingana wenyewe tunabishana weee mwisho tunafikia hitimisho,kwani hakuna hata siku moja tuliyowahi kupigana au kuchomeana nyumba kwa sababu ya kushindana kihoja.Hebu Mwanakijiji watolee thread zilizomo jf zichapwe kwenye magazeti watu wajue nini tunakisema mule kama kweli ugaidi ule,hivi kujadili lugha,sayansi,elimu siasa na uchumi ni ugaidi?Hawa polisi wanaambiwaa au mwema mwenyewe ashawahi kulog in na kuangalia nini kinasemwa mule?Aiiibu aibu ,waje tu watukamate lakini hatutasita kutoa maoni yetu kwa mujibu wa ibara ya 18 ya katiba. |
30. Jambo Forum vs Tanzania Polisi....NWA vs Written by Yebo Yebo, on 20-02-2008 23:21 Hii inanikumbusha miaka ya mwishoni mwa 80\'s ofisa mmoja wa FBI aliandika barua kutishia kikundindi cha muziki wa Rap kilichokuwa kinaibukia wakati huo cha NWA...kufuatia Barua hiyo umaarufu wa NWA ulizidi maradufu; kwa wale wapenzi wa muziki wa Rap watakuwa wanajua historia kamili.... Sasa hapa Polisi wetu badala ya kukamata wahalifu wao wanaenda kukamata watoto wanaotumia uhuru wao wa ujuzi kuwapa Watanzania uwanja wa kutoa maoni...mimi nina furaha haya yametokea maana sasa umma wa Watanzania utajua haki zao...kwa namna moja au nyingine Jambo Forum itarudi na Ari Mpya na Kasi Mpya tena kwa misaada na michango zaidi iliyoenda shule....this day long coming. God Bless Tanzania...God Bless Jambo Forum |
31. Shemeji Written by totoo, on 21-02-2008 01:39 Said Mwema, Shemeji wa JMK unategemea nini? |
32. IGP Mwema mbona unajiabisha hivyo? Written by MwanaJF mwandamizi, on 21-02-2008 07:09 Hivi hawa polisi wetu wataamka lini? Kutwa kuchwa kutumiwa kwa manufaa ya mafisadi hata kushtuka hawashtuki wanaona sawa tu, yaani mpaka IGP anadiriki kuongea pumba huku akijua kabisa anaongea pumba! Ukisikia wasaliti ndio hawa, badala ya kusimamia haki na usalama wa raia wao wanatanguliza matumbo mbele, watavuna walichopanda... |
33. Jamaa wameishiwa Written by TechMaro, on 21-02-2008 07:36 Hii ni kuonyesha jinsi gani serikali yetu inavyoongozwa... Ni tokea lini watu wasiheshimu nafasi ya wistleblowers katika jamii yao???badala to encourage with the warning kwamba ziwe moderated na za ukweli jamaa wanataka waifungie.... Hii ni aibu kwa serikali, inaonesha hawajui wanachotakiwa kukifanya. Sasa hivi wameungana na mafisadi ili kuhakikisha hakuna forum ya kuwaumbua in the future...Aibu tupu and akili ndogo sana.... |
34. JF imeshinikizwa ifungwe na kigogo wa je Written by TechMaro, on 21-02-2008 07:52 Aidha vijana wa CHADEMA tumesikitishwa na kutoweka hewani kwa mtandao wa Jambo Forum ambako kutokana na vyanzo mbalimbali inaelezwa kwamba waratibu wa mtandao huo wameshinikizwa kuufunga kutokana na shinikizo la ‘kigogo’ mmoja wa jeshi la polisi kwa maelekezo toka serikalini. Hii ni kutoka kwenye blogu ya Mnyika.....Hivi ndo ukweli huo?? Invisible, Mwanakijiji etc tuambiane ukweli.. |
35. jamani tuunganeni kuirudisha JF Written by FD, on 21-02-2008 07:58 Kweli inasikitisha. Inatakiwa mkuu wa polisi kabla hujongea kitu ufanye utafiti wa kina. Gaidi gani anasaini na jina lake? gaidi gani anatoa namba yake ya simu? And above all Magaidi gani wanapingana kila kukicha? Walichofanya ni kutaka wananchi wawe na hamu ya kujua kuna nini JF. |
36. Ukweli ni nini? Written by mama lao, on 21-02-2008 10:35 Jamani tuelezeni vizuri kitu gani hasa kinaendelea. JF mtandao wa "kigaidi"??? Inawezekana kweli??......au tutume SMS kwa Mkuu wa nchi???? |
37. Kuna Ukweli hapo.... Written by kibunango, on 21-02-2008 11:49 Yapo mazuri mengi yalifanywa na JF, lakini hivi karibu kumekuwepo na maneno ya uchochezi na ya kigaidi toka kwa memba kadhaa, bila ya kukaripiwa eitha na mod au wajumbe wenyewe. |
38. Written by Anzisheni mwingi, on 21-02-2008 11:58
 |
39. habari leo Written by DAR si LAMU, on 21-02-2008 13:29 ..gazeti la habari leo lina kichwa kikubwa cha habari "WALIOFICHUA UFISADI WAHOJIWA POLISI".....wadaiwa kukashfu na kufanya uchochezi. ..hili si ni gazeti la serikali? mengine hayajaandika or at least kutoa front page. baada ya bush kuondoka hili linaweza kuwa gumzo jipya. ..by the way,gumzo forum vipi? any life in there? |
40. INAKUWAJE POLISI................ Written by Mimi, on 21-02-2008 15:01 Kwanza kwa nini wamewaweka ndani hao vijana bila hata kujua sababu ya kuwawekea ndani. HAWA POLISI WAKASOME. wanawekaje ndani watu kwa kupokea tu kutoka kwa hao mafisadi. NINA WASI WASI RUSHWA INATEMBEA HAPO NINI?. Kwa nini wasiwaweke ndani wale waliotajwa kwenye ufisadi wa RICHMOND wakati uchunguzi mwingine unaendelea wanawakamata watu ambao ni wanyonge. Wajue MNYONGE MNYONGENI LAKINI HAKI YAKE MPENI. Dunia imeendelea hivyo nadhani hawa polisi inabidi wawe wanapitia mitandao mbali mbali ili waone uhuru wa habari ulivyo. YAANI VYOMBO VYA USALAMA NAVYO VINAENDESHWA NA WATU WENYE PESA. BASI HAO MAFISADI WAINUNUE HIYO POLISI IWE INAWAFANYIA KAZI HAO NA SIYO RAIA WANYONGE. |
41. Re: KIbunango!!! Written by Tata, on 21-02-2008 15:46 We Kibunango wewe labda ndio gaidi mwenyewe na chochezi peke yako! How dare you even say that? Wewe unataka kuambia watu kuwa nikweli JF ni ya magaidi? Do you even know what JF did to the best of Tz? Kama wewe ni mmojawapo wa watu waliokuwa wanaibia serikali, halafu unaogopa JF watakutolea siri zako hadharani, basi wewe sema tu lakini JF itarudi na with more power. By the way you must be one of them THIEVES!!!! |
42. mitandao mingi ya bongo inagoma vipi? Written by Re-nb, on 21-02-2008 15:51 Jamani leo hali ni mbaya mno, kwani nakosa habari za muhimu na burudani kwani JF tatizo linajulikana lakini hata habari za gazeti la Tanzania daima hazifunguki, pia bongo5 nayo hakuna vipi? tunakosa habari. by the way natoa pole kwa wana JF wote ila naamini kuwa ushindi utapatikana bila shaka.  |
43. Written by mwanakijiji, on 21-02-2008 16:16 Wewe Kibunango na wewe si memba pia, kama wengine ni maghaidi, kwanini wewe usiwe ni mmoja wao? Yawezekana kuwa ni wewe ndiyo umetoa maneno ya kighaidi kule Jambo Forums na baadaye kuwatonya rafiki zako kusema "unaona hawakunikemea"? Kama uliona kuna maneno au maoni ya kighaidi ulichukua hatua gani kuwajulisha ma MoD au wanachama wengine juu ya maneno hayo? |
44. Written by Roya Roy, on 21-02-2008 17:07 Kibunango, Magaidi hawasemi ila wanapenda kupanga na kufanya mashambulizi, mara nyingi ya uharibifu. |
45. Written by TM, on 22-02-2008 03:45 Bogus kabisa hawa watu!!! Wanachama, mimi naona kuna umuhimu wa kufungulia Polisi multi billion shilling lawsuit ama they should retract their statement. Munasemaje ? |
46. Si kazi ya Polisi kuhoji waliokashifu Written by FD, on 22-02-2008 07:08 Kibunango, Sio kazi ya polisi kuhoji waliotoa kashfa. ni kazi ya aliyekashifiwa kwenda mahakamani. Kesi za Daawa ni za daawa sio za kipolisi. Ningefurahia kuona polisi wakiwakamata mafisadi na sio wanaowataja mafisadi! Nchi haiendelei kwa kuwa tuna viongozi kama hawa. |
47. Written by mtafutaji, on 22-02-2008 10:19 duh naona jf sio mchezo. |
48. NAMBA YA MWEMA NA WENGINEO!! Written by KibangaAmpigaMkoloni, on 22-02-2008 11:11 BabaH,uliomba numbe ya mwema hii hapa Said Mwema 0754-785557 na nnyingine nyingi za wakuu wapolisi zinapatika kwenye website yao kwa link hii http://www.policeforce.go.tz/kuwasiliana.html Jamani JF irudi haraka kwani kazi bado aijaisha mafisadi bado wapo wanatanua wanadai UCHUNGUZI UNAENDELEA uchunguzi gani huo wakati kwenye ripoti kila kitu kipo wazi! |
49. kegycekd Written by kegycekd, on 07-03-2008 08:22 psxyxcax torbxbhi ejpudtpi http://oaonfczy.com fmnzoxvh roxylfhn |
50. Written by kapetto, on 14-03-2008 12:44 mimi ningeomba jeshi la polisi kuwa shuhulikia hawa watu walobainika kwamba wamekula rushwa na kubomoa nyumba za watu wa tabata bila serekali kujua lolote na imesha bainika kwamba milioni mia moja hakuna haja ya kuweka tume ni kifungo tu wanawafanya watanzani leo kuwa wakimbizi kwenye nchi yao kwa manufaa yao binafsi wala swala hili si lakunguja kesho inatiauchungu mnoo javascript:ac_smilie(' ') |
|